Header Ads

SHULE YA MSINGI YENYE VYUMBA VINNE VYA MADARASA NA WANAFUNZI KUANZIA DARASA LA KWANZA MPAKA LA SABA WILAYANI MAKETE HII HAPA

Shule ya Msingi Imehe iliyopo Kata ya Bulongwa ni miongoni mwa shule kongwe Wilayani Makete lakini bado inakabiliwa na uhaba mkubwa wa kutokuwa na vyumba vya Madarasa na kusababisha kufanya vibaya kwenye Matokeo ya Darasa la nne na la saba kila mwaka

Shule ya Msingi Imehe inajumla ya wanafunzi 137 kuanzia Darasa la kwanza mpaka Darasa la saba na inavyumba vinne tu vya Madarasa na inajumla ya walimu wanne wanaofundisha shuleni hapo,shule hiyo ilianzishwa mwaka 1976 ikiwa na jumla ya wanafunzi 30

Tokea kuanzishwa kwa shule hiyo imekuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya upungufu wa vyumba vya Madarasa hali inayopelekea wanafunzi kusoma kwa mlundikano jambo ambalo linaweza kusababisha wanafunzi kuugua magonjwa mbalimbali hususani ya kuambukiza na kusababisha kuwa na matokeo mabaya kwa wanafunzi

Kwa upande wa taaluma shule hiyo bado imekuwa na changamoto kubwa ya ufaulu duni kulingana na wanafunzi kushindwa kusoma katika Mazingira rafiki badala yake darasa moja linatumiwa na Madarasa mawili kwa wakati mmoja pamoja na baadhi ya wanafunzi kutembea umbali mrefu kulingana na Jiografia ya kijiji hicho kuwa na Milima mingi

Shule ya Msingi Imehe kwa sasa inauhitaji wa vyumba vitano vya Madarasa ili kukidhi idadi ya Wanafunzi na vyumba vya kusomea pamoja na kuwa na ofisi ya walimu

Mpango uliopo hivi sasa katika kukabiliana na hali hiyo ni kupata vyumba viwili vya Madarasa pamoja na ofisi moja ya walimu vyenye thamani ya shilingi Milioni 50 mchango unaotarajiwa kuombwa/kukusanywa kutoka kwa wadau mbalimbali wakiwemo wazawa wa kijiji cha Imehe waishio ndani ya nje ya kijiji hicho,Taasisi mbalimbali,Serikali pamoja na nguvu za wananchi wenyewe

Wananchi,Wazaledo na wadau wa Maendeleo na wapenda Elimu Wilayani Makete mnaombwa kusaidia katika ujenzi wa vyumba hivyo viwili vya Madarasa ili kunusuru hali iliyopo katika shule hiyo kwa kupunguza mlundikano wa wanafunzi Darasani na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa shule hiyo ya Msingi Imehe

Mwonekano wa Majengo ya shule ya Msingi Imehe

 Hiki ni chumba kinachotumika kama Darasa lakini pia kinatumika kama stoo ya shule hiyo
Mwonekano wa chumba kimojawapo kwa ndani kinachotumika kuwafunzia wanafunzi wa shule ya Msingi Imehe

Mandhari ya kijiji cha Imehe

No comments

Powered by Blogger.