Header Ads

NAMNA AMBAVYO MARIA NA CONSO WALIVYOFARIKI KWA MPISHANO WA DAKIKA KATI YA 10 NA 15



Mganga mfawidhi Hospitali ya Rufaa Iringa Museleta Nyakiroto ameeleza namna ambavyo safari ya Maria na Consolata ilivyokuwa “Mnamo tarehe 17 May 2018 majira ya saa moja nusu jioni wakiwa wametokea Hospitali ya Taifa Muhimbili walikokuwa wakipatiwa Matibabu baada ya kuruhusiwa lakini waendelea kupata Matibabu wakiwa nyumbani”

“Rufaa ya iringa tulitakiwa kuendelea kufanya ufatiliaji kwa Maria na Conso wakiwa nyumbani,kwa hiyo walifikishwa Iringa na Ambulance na walisindikizwa na Daktari,Muuguzi mmoja na Technical mmoja wa Mambo ya ICU kwa ajili ya ile mitungi ya gesi ambayo wamesafiri nayo, kwa hiyo lengo lao na letu ilikuwa ni kuwapumzisha ili wakipumzika basi waruhusiwe kwenda  nyumbani” 

“Kwa hiyo tangu hiyo tarehe 17 May tumekuwa tukiwahudumia hapa rufaa Iringa wakiendelea kupata matibabu mbalimbali ikiwemo Oxygen kwa hiyo tangu siku hiyo hatukuona kama wanapata unafuu sasa mpaka jana ilipofika majira kati ya saa 2:30 mpaka saa 3 usiku wakawa wamefariki”

“Aliyenza kufariki ni Maria baadaye Consolata naye akawa amefariki walipishana dakika kumi mpaka kumi na tano hivi”

No comments

Powered by Blogger.