Header Ads

BARABARA YA LAMI CHIMALA-MATAMBA-KITULO IPO KWENYE MCHAKATO


Image result for norman sigalaSerikali imesema Ujenzi wa Barabara ya Lami kutoka Chimala kupitia Matamba mpaka Kitulo ni Muhimu kwa Maendeleo ya nchi na wananchi wa Makete ikiwa ni pamoja na Hifadhi ya Taifa ya Kitulo iliyopo Wilayani Makete Mkoani Njombe

Serikali imesema kwa sasa inamchakato wa kuboresha Barabara zilizomo kwenye hifadhi za Taifa ikiwemo barabara ya Chimala,Matamba –Kitulo na Wizara ya Maliasili na Utalii  kwa kushirikiana na Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na uchukuzi imesema itaendelea kuona umihimu wa Barabara hiyo kama Mh.Norman Sigalla King Mbunge wa Jimbo la Makete alivyoomba Barabara hiyo iweze kujengwa kwa Kiwango cha Lami

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Wizara ya Maliasili na Utalii Mh.Hasunga Bungeni jijini Dodoma hapo jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Makete Mh.Prof.Norman Sigalla King aliyetaka kujua Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Lami kutoka Chimala-Matamba mpaka kitulo kwa manufaa ya wananchi wa Maeneo hayo na kukuza utalii katika hifadhi ya Taifa ya Kitulo


1 comment:

Powered by Blogger.