Header Ads

WANAFUNZI MSIKUBALI KURUBUNIWA NA MIATANOMIATANO:MONNY LUVANDA



 Wanafunzi na Vijana wa Kike Wilayani Makete Mkoani Njombe wametakiwa kuwa wawazi katika masuala ya Mahusiano na kutojiingiza katika Mapenzi katika umri usiowaruhusu na kuzingatia Masomo kwa wale walioko Shuleni

Naibu Katibu wa Chama cha Maendeleo Makete(MDA) Bi.Monny Luvanda akizungumza na wanafunzi wanaosoma Mang'oto Sekondari

Akizungumza na wanafunzi pamoja na Vijana waliofika shule ya Sekondari Mang’oto iliyopo kata ya Mang’oto Wilayani hapa Naibu Katibu wa Chama cha Maendeleo Makete(MDA) Bi.Monny Luvanda ambaye pia ni Mzazi na Mlezi wa watoto amesema inaleta taswira mbaya kwa Vijana kujiingiza kwenye masuala ya Kimapenzi katika umri wa chini ya miaka 18 na ukizingatia wengi wao kwa umri huo wanakuwa Mashuleni na sheria inazuia kujihusisha kimapenzi katika Mazingira hayo

Pia Bi.Monny Luvanda ameongeza kuwa Mabinti wengi huwa wanarubuniwa na Vijana wa Mitaani kwa miatano miatano ambazo ni danganyatoto kwani Mambo hayo yanapita na watakuja kuyaona Mtaani wakati wao ukifika

“Mkipata Mimba au Ukimwi katika umri huu na mkaanza kuugua nani atapaswa kumuhudumia mwezie kati ya wewe mtoto na Mzazi? Aliwauliza wanafunzi ambao walimjibu kwa kusema sisi ndio tegemeo na siyo Mzazi kuanza kumuuguza tena mwanaye”

“Mtoto unatakiwa ujilinde,usimame katika nafasi yako ili uje kuwa Faraja kubwa kwa Mzazi wako hapo baadaye,Nawaomba Muangalie kilichowaleta hapa shuleni ni Masomo tuu”

“Ukiona mtu anakusumbua kuwa muwazi mwambie hata Mwalimu au mzazi kuwa kuna mtu ananisumbua ili usije kukatisha masomo yako bure kwa kupewa ujauzito au kuambukizwa magonjwa,Wanangu,wadogo zangu haya mambo yapo tu na yanapita tafadhali sana someni kwa bidii”

Bi.Monny Luvanda alimaliza kusema “Elimu ni Mkombozi wa Maisha yenu na Mungu awabariki sana niwatakie Amani ya Mungu AMINA”

No comments

Powered by Blogger.