Header Ads

SERIKALI IPO MBIONI KULETA PUNDAMILIA HIFADHI YA TAIFA KITULO


Image result for hifadhi ya kitulo

Maua yakionekana na mwonekano wa kuvutia katika Hifadi ya Taifa Kitulo


Wananchi Wilayani Makete Mkoani Njombe wametakiwa kuzitumia fursa za kuwekeza katika Hifadhi ya Taifa ya Kitulo.

JOFREY WILSONI  KYANDO ni moja kati ya Viongozi kutoka Hifadhi ya Taifa Kitulo amesema ndani ya Hifadhi hiyo kuna fursa za uwekezaji kwa Wananchi  ikiwemo kujenga Nyumba za kulala wageni pamoja na kujenga sehemu za kupiga  mahema kwa ajili ya kulala wageni ndani ya Hifadhi hiyo.

JOFREY WILSONI  KYANDO amesema ‘‘Fursa kubwa tuliyonayo katika hifadhi ya kipekee ni kivutio kikubwa ambacho hakipatikani kwenye hifadhi nyingine yeyote i ni maua lakini tunayo fursa nyingine ya uwekezaji ni kujenga Hoteli za Kisasa,kujenga Lodge na kujenga sehemu za kupiga Mahema kwa ajili ya watalii Fursa hizo ziko wazi kwa Watanzania wote na watu wengine kutoka nje ya Tanzania”

“Kwa hiyo tunapenda kuchukua fursa hii ya Utalii kwa watu wote bila ubaguzi kwa ajili ya kukuza uchumi wa Nchi yetu pendwa ya Tanzania”

Bwana JOFREY  amewatoa hofu wanamakete na Tanzania kuondokana na dhana ya kusema kuwa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo haina wanyama ilihali Hifadhi ina wanyama wadogo wadogo na hivi karibuni hifadhi hiyo ipo mbioni kuleta wanyama wakubwa wakiwemo pundamilia.
Image result for hifadhi ya kitulo


Hifadhi ya kitulo ni moja kati ya hifadhi kumi na sita Nchini na ni Hifadhi inayosifika kuwa na kivutio  kikubwa na cha kipekee cha maua    ambacho hakipatikani katika Hifadhi yeyote ile.

Pia unaweza kufanya utalii wa kutembelea maporomoko ya Maji,kupiga mahema,Utalii wa picha,kuona wanyama wadogowadogo kama digidigi,swala,nyani,utalii wa kutembea kwa miguu vitu vingine vingi

Kwa Mtanzania ni Muhimu sana kutembelea Hifadhi za Taifa ili kujionea maajabu mengi na yenye kuvutia katika Hifadhi zilizopo hapa Nchini
Hifadhi ya Taifa ya Kitulo ni Hifadhi ya Taifa la Tanzania iliyopo katika Mkoa wa Njombe na Mbeya,ambapo awali ilijulikana kama Elton Plateau baada ya Mvumbuzi Fredrick Elton kupitia eneo hilo mnamo mwaka 1870
Mwaka 1960 Shirika la Chakula na Kilimo (FAO) lilichukua eneo hili kwa ajili ya ukulima wa ngano na ufugaji wa kondoo.
Baadaye likageuzwa kuwa shamba la ng'ombe ambalo lipo hadi leo. Kutokana na umuhimu wa eneo hili wadau mbalimbali wa mazingira walipendekeza eneo hili litangazwe kuwa hifadhi ya taifa ili kulinda umaridadi wa maua na mimea adimu inayopatikana ndani ya eneo hili.
Mwaka 2005, Kitulo ilitangazwa rasmi kuwa hifadhi ya Taifa ikijumuisha sehemu ya eneo la shamba la mifugoMsitu wa Livingstone na bonde la Numbi kiasi cha kilometa za mraba412.9 ndani ya mwinuko wa mita 2100 na 3000 juu ya UB.
Hifadhi hii inasifika kwa kuwa na maua aina mbalimbali na zaidi ya aina 30 hupatikana Kitulo pekee na maeneo kusini mwa Tanzania.
Maua ya Kitulo
Pia ndilo eneo pekee Tanzania ambapo ndege aina ya Tandawili machaka (Denhams Bustard) wana makazi. Wapo aina mbalimbali ya ndege kama vile Mpasua mbegu mweusi(Kipengere seed eater) na wengineo.
Jamii mpya ya nyani (Lophocebus Kipunji) waligunduliwa mwaka 2003 Kitulo. Hifadhi hii ina uwanda wa tambararemabondevilima na maporomoko ya maji. Ndani ya msitu, kuna miti aina ya cidar yenye urefu wa zaidi ya mita 50 na inakadiriwa kuwa mirefu kuliko yote duniani.
Kitulo inafikika kwa gari kutoka Chimalakilometa 78 mashariki kwa mji wa Mbeya. Pia unaweza kufika ukitokea Zambia kupitia Tunduma au Malawi kupitia Karonga kwa barabara.
Reli ya TAZARA hupita karibu na hifadhi ya Kitulo.

No comments

Powered by Blogger.