Header Ads

ASKOFU MTEULE KKKT-DKK MAKETE ATOA PONGEZI KWA CHAMA CHA MAENDELEO MAKETE (MDA)


Askofu Mteule Dayosisi ya Kusini Kati Wilson Sanga amewataka wanaMakete kushirikiana katika kuiletea Maendeleo Wilaya ya Makete bila kujali itikadi zao za Kidini huku akiumwagia sifa Ushirikiano walionao WanaMakete waishio ndani na nje ya Makete kupitia Chama cha Maendeleo Makete MDA kwa shughuli mbalimbali zinazofanywa na Chama hicho katika Wilaya hii

Askofu Mteule Sanga ameyasema hayo Mapema wiki hii wakati wa Mazungumzo ya Pamoja kati yake na Viongozi wa Chama cha Maendeleo Makete MDA sambamba na Baraza la Viongozi wa Dayosisi hiyo ya KKKT DKK Makao Makuu ya Dayosisi hiyo Makete Mjini Mkoani Njombe

Askofu Mteule Wilson Sanga amesema kupitia Chama cha Maendeleo Makete (MDA) na WanaMakete Mbalimbali waliyoungana kupitia Mitandao ya Kijamii kama Makundi ya WatsApp wamejiunga katika kusaidia shughuli mbalimbali za Maendeleo Makete na kwenye Dayosisi hiyo ili kuangalia namna bora ya kuboresha Huduma mbalimbali zinazotolewa na Dayosisi hiyo Kielimu,Kiafya na hata Kidini katika Kuibua na kuendeleza Miradi inayosimamiwa na Dayosisi hiyo

Wakati huo huo Askofu Mteule ameipongeza MDA kwa Mchango mkubwa walioutoa Shule ya Sekondari Mang’oto kwa kutoa vifaa mbalimbali vya ujenzi wa Bweni la Wavulana na kuongeza kwamba Kanisa pia linamchango wake mkubwa katika shule ya Sekondari Mang’oto hivyo kwa kufanya hivyo wamelisaidia Kanisa pia

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Maendeleo Makete MDA Wakili Philipo Mahenge akizungumza na Askofu huyo Mteule,Msaidizi wa Askofu pamoja na Baraza la Uongozi wa Dayosisi hiyo amesema nia ya MDA ni kuongeza ushirikiano baina ya Chama hicho na Taasisi Mbalimbali zikiwemo za Kidini katika Kuiletea Maendeleo Wilaya ya Makete

Pia amewapongeza waumini wa Dini hiyo ya Kikristo kwa Uchaguzi uliofanyika katika kumpata Baba Askofu Mteule Wilson Sanga

Kwa upande wake Msaidizi wa Askofu Mch.Adili Pagalo amewapongeza WanaMakete kwa kuungana kupitia Chama cha Maendeleo Makete MDA kwa shughuli mbalimbali wanazozifanya ambazo ni za Kimaendeleo kwa Wilaya ya Makete,huku akiwataka WanaMakete waishio Nje ya Makete kuwa na kumbukumbu ya kurudi kwao na kuwekeza kwenye Miradi ya Maendeleo ili kuikuza Makete Kiuchumi

Award Mpandila ni Katibu wa Chama cha Maendeleo Makete (MDA) amesema MDA siyo Chama cha Kisiasa na MDA imeamua kushirikiana na Taasisi mbalimbali zikiwemo za Kidini hivyo Chama kinajipanga kuhakikisha kinawaunganisha WanaMakete katika kuleta Maendeleo Makete kupitia ushirikiano kutoka kwa Wadau Mbalimbali wa Maendeleo

Na katika Sherehe zinazotarajiwa kufanyika mwezi ujao za kumuweka wakfu Askofu Mteule Mdau wa Maendeleo Makete Bw.Award Mpandilah ameahidi kuchangia kiasi cha shilingi Laki moja kwa ajili ya kusaidia Maandalizi ya sherehe hiyo ya kuwekwa wakfu kwa Baba Askofu
 Kutoka kushoto ni Katibu wa MDA Award Mpandila,akifuatiwa na Askofu Mteule Wilson Sanga,Katikati ni Naibu Katibu wa MDA Bi.Monny Luvanda,wapili kulia ni Wakili Philipo Mahenge na wa kwanza Kulia ni Msaidizi wa Askofu KKKT-DKK Mch.Adili Pagalo
 Askofu Mteule KKKT-DKK Wilson Sanga Kulia akisoma Katiba ya Chama cha Maendeleo Makete(MDA) baada ya kukabidhiwa na Makamu Mwenyekiti wa MDA Philipo Mahenge
 Askofu Mteule KKKT-DKK Wilson Sanga kushoto akisikiliza jambo kutoka kwa Viongozi wa MDA hawapo pichani akiwa na Baraza lake 
Award Mpandila akizungumza wakati wa Mazungumzo ya Pamoja kati ya Viongozi wa Chama cha Maendeleo Makete MDA sambamba na Baraza la Viongozi wa Dayosisi hiyo ya KKKT DKK Makao Makuu ya Dayosisi hiyo Makete Mjini 



No comments

Powered by Blogger.