Header Ads

MAPAO YAANZISHA KLABU ZA WASAIDIZI WA KISHERIA MASHULENI


Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Iwawa ambao ni wanachama wa Klabu ya Wasaidizi wa Kisheria wakiwa katika picha ya Pamoja na Walimu walezi,Mkurugenzi wa MAPAO na Mjumbe wa Bodi ya MAPAO

Shirika la Wasaidizi wa Kisheria Wilayani Makete (MAPAO)limeanza kutoa Elimu ya Kisheria kwa Wanafunzi Shule za Sekondari na Msingi na kuunda Klabu za Wasaidizi wa Kisheria kwa Wanafunzi hao

Akizungumza na Kitulo Fm Mkurugenzi Mtendaji Shirika hilo Wilaya ya Makete Denis Sinene amesema kuanzishwa kwa Klabu za Wasaidizi wa Kisheria kwa Shule za Sekondari na Msingi ni Mpango endelevu kwa ajili ya kutoa Elimu ya Msaada wa Kisheria kwa shule zote za Sekondari na Msingi zilizopo Wilayani hapa na nje ya Wilaya

"Kwa sasa tayari tumeanza mchakato wa kufungua Klabu za Wasaidizi wa Kisheria kwenye shule zetu za Sekondari na Msingi na kwa kuanzia tumeanza Iwawa Sekondari ambayo inawanafunzi Zaidi ya mia saba na siyo kwamba wote wapo kwenye Klabu hiyo bali wachache kama hamsini hivi ndio wapo kwenye Klabu hiyo na hao watakuwa Mabalozi kwa wengine kwa kutoa Elimu ya Msaada wa Kisheria kupitia Vipindi mbalimbali na Sanaa"Alisema Mkurugenzi huyo Denis Sinene

"Pia siku chache zijazo tutafungua Klabu nyingine kwa Shule yoyote ya Msingi kutoka kata ya Lupalilo au Isapulano kwenye Shule yoyote itakayoteuliwa"Aliongeza Sinene

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa uanzishwaji wa Klabu hizo unalenga kuimarisha uelewa wa Wanafunzi kuhusu Sheria Mbalimbali zinazowahusu na Wanafunzi hao watakuwa Mabalozi wazuri kwa Wazazi/walezi wao ambao wanauhitaji na Msaada wa Kisheria watakuja kwa wingi zaidi MAPAO ili kupata Msaada wa Kisheria

Pia ameongeza kuwa uanzishwaji wa Klabu hizo Mashuleni utaleta unafuu kwa wanafunzi kutambua Sheria ambazo zitaweza kuwasaidia Shuleni na katika Maisha yao ya hapo baadaye na wengine huenda wakatimiza ndoto zao za kuwa Wanasheria hapo baadaye

Mkurugenzi huyo amesema kwa sasa Elimu ya Msaada wa Kisheria itaendelea kutolewa kwa Wanafunzi shule zote za Sekondari na Msingi ili kuwajengea uwezo wanafunzi wa kutambua Haki zao na Sheria kwa ujumla wake
 Walimu walezi wa Klabu ya Wanafunzi wasaidizi wa Kisheria Iwawa Sekondari

Wanafunzi Viongozi wa Klabu hiyo ya wasaidizi wa Kisheria Iwawa Sekondari

No comments

Powered by Blogger.