Header Ads

WATENDAJI WA VIJIJI 50 KATI YA 53 WALIOACHISHWA KAZI WAREJESHWA KAZINI WILAYANI MAKETE


Watendaji 50 kati ya 53 wa vijiji waliosimamishwa kazi kwa kukosa sifa za ufaulu wa  kidato cha nne Wilayani Makete Mkoani Njombe wameripoti Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Makete kwa ajili ya kuendelea na kazi
Kufuatia agizo la waziri wa nchi ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma na Utawala bora KAPTEN Mstaafu GEOGY MKUCHIKA utekelezaji wake umeanza
Afisa Utumishi  Wilaya ya Makete Bw.ASUKILE MBOGELA

Akizungumza na Kitulo Fm Mapema hii leo juu ya kuripoti kwa Watendaji hao wa Vijiji Afisa Utumishi  Wilaya ya Makete Bw.ASUKILE MBOGELA amesema tayari Watendaji 50 wamesha ripoti katika halmshauri ya Wilaya ya Makete Mkoani Njombe kwa ajili ya kuendelea na majukumu yao huku watendaji wengine watatu wakiwa hawajaripoti kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kustaafu,kugushi Cheti na mmoja kufariki dunia.

ASUKILE MBOGELA amewatoa hofu Watendaji hao wa Vijiji juu ya mishahara yao ambayo hawajapata kwa kipindi chote ambacho walisimamishwa kazi na amewataka kusubiri mara baada ya kujaza fomu maalumu kwa kufuata taratibu watapatiwa  Mishahara hiyo.

Huku akiwataka watendaji hao ambao wanarejea kazini kufanya kazi kwa weledi kwa kufuata kanuni na taratibu za utumishi wa umma zinavyowataka



No comments

Powered by Blogger.