Header Ads

MNYAMA KIBOKO ASHAMBULIA MASHAMBA NA KUHARIBU ZAO LA MPUNGA WILAYANI MAKETE


Zaidi ya Wakulima 15 Zao la Mpunga  Kijiji cha Ruaha kilichopo Kata ya Mfumbi Wilayani Makete Mkoani Njombe mashamba yao yameharibiwa vibaya na mnyama Kiboko.
Image result

Afisa Kilimo wa Kijiji cha Ruaha Kata ya Mfumbi Bw.HAMISI MKULICHE amesema wakulima 15 Mazao ya wakulima hao hasa zao la mpunga ambalo linalimwa kwa wingi kijijini hapo yameharibiwa vibaya kufuatia uharibifu unaofanywa na mnyama huyo

Bwana HAMISI MKUCHIKA amewataka wakulima kuwa wavumilivu kwani suala la kumtoa mnyama huyo katika mashamba hayo linafanyiwa kazi huku akiwataka wakulima kuwa makini wanapokwenda Mashambani mwao ili wasijeruhiwe na mnyama huyo

Wakulima wa Mpunga kijijini hapo wamesema Mnyama huyo amekuwa kishinda kwenye mashamba yao na kuharibu Mazao mbalimbali hususani Mpunga kwa zaidi ya wiki mbili sasa na kuziomba mamlaka husika kuchukua hatua za kumuondosha mnyama huyo kwenye mashamba yao

Naye Afisa Utalii Wilaya ya Makete Idara ya Ardhi na Maliasili JOSHUA MUOGORO amesema kwa eneo lolote ambalo linatukio la wanyama kuvamia mashamba ya wakulima wanatakiwa kutoa taarifa kwa Mkurugenzi Mtedaji Wilaya ili Idara ya maliasili waweze kulishughulikia.

Bwana Joshua amewataka wananchi kutambua kuwa tatizo kama hilo linapotokea hakuna fidia kwani eneo hilo ni mapito kwa wanyama na amewataka wananchi kuchukua tahadhari kwani  maliasili wameanza utaratibu wa kushughulikia tatizo hilo

No comments

Powered by Blogger.