TUTAIHUBIRI INJILI POPOTE ULIMWENGUNI:-KWAYA YA NEEMA MAKETE MJINI
Mwenyekiti wa kwaya ya Neema Ndg.Fadhili Nkenza akizungumzia maandalizi ya Uzinduzi huo akiwa katika Studio za KituloFM Redio jana Jumapili kwenye kipindi cha Faraja yako
Kwaya
ya Neema (KKKT-DKK) Makete Mjini inayofuraha kuwakaribisha wananchi wote katika
uzinduzi wa DVD yao yenye jina lililobeba Album nzima ya “YESU MPONYA” mnamo
tarehe 29 April 2018
Katika
Uzinduzi huo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa ni Mwanamichezo maarufu nchini
Ndg.Clement Sanga ambapo uzinduzi huo utafanyika Kanisa la KKKT Usharika wa Makete Mjini
kuanzia saa 8:00 Mchana baada ya Ibada
Kwaya
Mbalimbali zitakuwepo katika kusindikiza Uzinduzi huo ikiwemo kwaya ya Haleluya
kutoka Iyunga Mbeya,Amkeni Kwaya kutoka Isapulano,Kwaya ya Wito kutoka Amani
Bulongwa,Kwaya ya Kati Tandala,Mt.Cesilia
Makete Mjini,Uvikanjo Makete Mjini,Kwaya ya Mwimbieni kutoka Bulongwa,Hosiana
Kwaya kutoka Bulongwa,Kwaya ya Zaburi Idunda,Kwaya ya Ipelele na Waimbaji
mbalimbali akiwepo Samsoni Kabiki,Aldo Sanga na wengine wengi watakuwepo
Mwenyekiti
wa Kwaya hiyo Ndg.Fadhili Nkenza amesema kwaya hiyo imetoka mbali mpaka kufikia
katika hatua ya uzinduzi huo pamoja na kukumbana na changamoto mbalimbali
lakini walikuwa wakimtegemea Mungu wakati wote katika kazi hiyo
Nkenza
amesema Uzinduzi wa Album hiyo ya DVD ni wa kwanza kufanyika kwa Kwaya hiyo
tokea kuanzishwa kwake na malengo ni kuhubiri neno la Mungu kwa njia ya uimbaji
popote ulimwenguni
Pia
ameongeza kwamba wao kama kwaya wanajipanga kuwa na Website au Blog kwa ajili
ya kusambaza kazi zao kupitia mitandao ya Kijamii ili kila mtu aweze kupata
nyimbo zao kwa njia rahisi popote atakapokuwa
Angalia hapa chini picha za baadhi ya waimbaji wa kwaya hiyo wakiwa Studio za KituloFm Redio jana Jumapili
No comments