MWENYEKITI WA CHADEMA WILAYA YA MAKETE AWATAKA WANANCHI KUSHIRIKIANA KATIKA SHUGHULI ZA MAENDELEO BILA KUBAGUANA
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Makete Ndg.Ibrahim Ngogo amewataka wananchi wa kata
ya Ikuwo na wanaMakete kwa Ujumla kushirikiana katika shughuli za Maendeleo
bila kujali itikadi za Kisiasa katika kuiletea Maendeleo Wilaya ya Makete
Ndg.Ibrahim Ngogo Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Wilaya ya Makete
Ndg.Ibrahim Ngogo ametoa rai hiyo wakati akizungumza na Wanachama wa Chama hicho kata ya Ikuwo kwenye mkutano wa ndani huku akiwasihi wananchi kwamba Siasa bila vitendo haziwezi kuleta Maendeleo hivyo wananchi wanatakiwa kushirikiana Pasipo kubaguana kwa itikadi za Vyama badala yake washiriki kikamilifu katika shughuli zote na Maendeleo
Wakati huohuo Ngogo amesema kama mtu atakataa
kuchangia mchango wowote wa shughuli za Maedendelo kisa Itikadi za Kichama basi
huyo haitakii mema Wilaya yake
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA)Wilaya
ya Makete Mh.Beatrice Kyando ameipongeza Serikali ya Awamu ya tano kwa
uwajibikaji huku akisema ushirikano baina ya Viongozi uendelee ili kuleta
Maendeleo
Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA)Wilaya ya Makete Mh.Beatrice Kyando
Wakati huohuo amewataka wananchi wa kata ya Ikuwo kumuombea Diwani wa kata hiyo na kushirikiana naye katika shughuli za Maendeleo ili kufanikisha Malengo ya kuwatumikia wananchi wake waliomchagua
Wakati huohuo amewataka wananchi wa kata ya Ikuwo kumuombea Diwani wa kata hiyo na kushirikiana naye katika shughuli za Maendeleo ili kufanikisha Malengo ya kuwatumikia wananchi wake waliomchagua
Katika Hatua nyingine Mh.Beatrice Kyando
amewataka wanawake wa kata ya Ikuwo na kata zingine Wilayani Makete kuunda
vikundi vya ujasiriamali vitakavyowasaidia kuinuana kiuchumi na siyo kubaki
kuwa tegemezi kwa waume zao
No comments