Header Ads

TFDA YATOA TAHADHARI KUHUSU BIDHAA


Image may contain: 1 person, standing and outdoor
Afisa  afya Wilaya ya Makete Ndg.Boniface Sanga

Wafanyabiashara Wilayani Mkoani Njombe wametakiwa Kutohifadhi Mafuta ya Kupikia,Chumvi,Maji, pamoja na Unga kwenye jua   ili bidhaa hizo zisipoteza ubora wake.

Agizo hilo limetolewa na Mamlaka ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA) Kupitia kwa Afisa  afya Wilaya ya Makete BONIFACE SANGA amesema bidhaa hizo hazitakiwi kukaa kwenye jua ilihali zinatakiwa kukaa sehemu ambayo ina ubariki ili zisipoteze thamani yake na kuleta madhara kwa binadamu.

‘‘Masharti ya hizo Bidhaa inatakiwa kukaa kwenye Baridi siyo kukaa juani ili zisiondolewe uthamani wake na kuleta madhara kwa watumiaji wa bidhaa hizo na  mfanya biashara yoyote ambaye atakiuka utaratibu huo atafungiwa biashara yake au bidhaa zake zitateketezwa kwa moto’’ Amesema Bonifasi sanga.

Hata hivyo BONIFACE SANGA amesema ndani ya siku kumi na nne [14] Idara ya Afya Wilaya ya Makete  watapita Kufanya Ukaguzi kwa wafanyabiashara ambao wanaweka bidhaa hizo kwenye jua endapo mfanyabiashara yeyote atakiuka utaratibu huo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi  yake.

Hatua hizo ni kutokana na sheria ya mwaka 2003 kifungu namba 19 sura ya 219 inayosimamia uharibifu wa  bidhaa hizo katika maeneo ya biashara na kuweka  kwenye jua ambapo virutubisho vyake vinaondolewa kwa kukaa kwenye jua.

Mamlaka ya chakula na dawa Tanzania  TFDA kwa Kushirikiana na Idara ya Afya Wilaya ya Makete imewaomba wananchi wilaya kuwa makini kutumia bidhaa hizo na Wafanyabiashara kuzingatia Taratibu na Sheria zinazotolewa na mamlaka husika ili kufanya Biashara kwa Uhuru.  

No comments

Powered by Blogger.