Header Ads

MTOTO WA DARASA LA KWANZA ATWEKWA NA MWANAMKE WANGING'OMBE MKOANI NJOMBE


Image result for KAMANDA RENATHA MZINGA
Kamanda Renatha Mzinga kulia

Jeshi la polisi Mkoa wa Njombe linamshikilia Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la COLLETHA NG'UMBI mkazi wa wilaya ya Wanging'ombe kwa kosa la kumteka mtoto mdogo anayefahamika kwa jina la ERICK HOSEA MTEWELE mwanafunzi wa darasa la kwanza wilayani hapo, na kuwataka wazazi wa mtoto huyo kutoa pesa ili waweze kurejeshewa mtoto wao.


Akizungumza na waandishi wa habari  kamishna msaidizi mwandamizi wa jeshi la polisi mkoa wa Njombe RENATHA MZINGA,amesema kuwa tukio la kutekwa kwa mwanafunzi huyo lilitokea mnamo tarehe 11 mwezi wa 4 mwaka 2018 wilayani hapo wakati mwanafunzi akirudi nyumbani.

Kamanda Mzinga amesema kuwa wakati shughuli za upelelezi zikiendelea ili kumpata mtoto huyo, Baba mtoto aitwaye WILLIAM MTEWELE alianza kupokea ujumbe mfupi uliomtaka mzee huyo aweze kutoa pesa kiasi cha shilingi laki 8 ili mtoto aweze kurejeshwa.

Aidha kamanda huyo wa polisi anasema kuwa jeshi la polisi mara baada ya kuendelea kufanya upelelezi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa na mtoto wake mwenye umri wa miaka miwili katika   wilaya ya mbarali mkoani Mbeya.

Katika hatua nyingine Kamanda mzinga amesema mara baada ya kukamatwa kwa mwanamke huyo amedai kuwa alimchukua mtoto huyo na kutaka kiasi hicho cha pesa ili aweze kulipa kiasi cha mahali alichokuwa akidaiwa na wazazi wake na hivyo mpaka sasa jeshi la polisi linaendelea kumhoji mwanamke huyo.​



No comments

Powered by Blogger.