Header Ads

WATUMISHI JIENDELEZENI KIELIMU HUSUSANI WALIMU:-ANTONY MPILUKA


Watumishi wa Umma Wilayani Makete Mkoani Njombe wametakiwa kujiendeleza Kielimu ili kuendana na Utendaji wa kisasa wenye kuzingatia Elimu na Teknolojia zaidi


Kutoka kulia ni Mwl.Mstaafu Jonick Ngogo aliyekuwa anaagwa,wa pili kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi H/w ya Makete Eliabu Simba na watatu kutoka kulia ni Mwl.Antony Mpiluka aliyekuwa anaagwa mara baada ya kustaafu wakiwa katika ukumbi wa Mikutano wa H/w Makete

Rai hiyo imetolewa mwishoni mwa juma hili na Aliyekuwa Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Makete Mwl.Antony Mpiluka akiwa katika hafla fupi ya kuagwa yeye pamoja na Mratibu Elimu Tarafa ya Matamba Mwl.Jonick Ngogo baada ya muda wa Kustaafu utumishi wa Umma kufika

Mwl.Antony Mpiluka amesema suala la walimu na watumishi wengine kujiendeleza kielimu ni jambo muhimu sana kwa Mazingira ya Ulimwengu wa Kisasa kulingana na umuhimu wa Elimu inavyozidi kuboreshwa

Mwl.Antony Mpiluka ameongeza kuwa ushirikiano kati ya watumishi ni muhimu katika kuboresha utoaji na upatikanaji wa Huduma,pamoja na kustaafu ameahidi kuendelea kushirikiana na watumishi akiwa kama Mzee mstaafu 

Kwa upande wake Mratibu Elimu Tarafa ya Matamba Mwl. Jonick Ngogo naye akiwa katika hafla hiyo ya kuagwa iliyofanyika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete amesema pamoja na kuwa amestaafu lakini ataendelea kutambua mchango wake Serikalini na kuendelea kutoa ushirikiano kwa watumishi wengine huku akiwashukuru watumishi wa Matamba na watumishi wengine waliokuwa wakishirikiana pamoja katika majukumu mbalimbali ya kijamii na kiserikali

Kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Makete Fransis Namaumbo,Ndg.Eliabu Simba amewasihi wastaafu hao kuendelea kuishi maisha ya kumtumaini Mungu na uwajibikaji ili kuendana na hali halisi ya Maisha ya uzeeni na kuishi vizuri na jamii inayowazunguka

Baadhi ya Watumishi waliohudhuria hafla hiyo ya kumuaga Afisa Elimu Wilaya ya Makete Mwl.Antony Mpiluka na Mratibu Elimu Tarafa ya Matamba Mwl. Jonick Ngogo wamewamwagia sifa wastaafu hao kwa utumishi wao uliotukuka kazini na kuwaomba watumishi wengine kuiga mifano ya wazee hao
Baadhi ya watumishi wakiwa katika ukumbi wa H/w Makete kwenye hafla ya kuwaaga Afisa Elimu Msingi Mwl.Antony Mpiluka na Mratibu Elimu Tarafa ya Matamba Mwl. Jonick Ngogo 
Mwl.Antony Mpiluka aliyesimama akiwa katika majukumu yake kabla ya kustaafu pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Makete Ndg.Fransic Namaumbo
Aliyekuwa Mratibu Elimu Tarafa ya Matamba Mwl. Jonick Ngogo mapema mwaka huu akikabidhiwa Zawadi na Bank ya NMB Tawi la Makete kwa kufaulisha vizuri wanafunzi shule za Msingi kwenye Tarafa yake 

No comments

Powered by Blogger.