Header Ads

RAIS MAGUFULI AKUBALI KINANA KUJIUZULU...... TAZAMA HAPA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA NEC YA CCM

Katibu mkuu Taifa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana ameng'atuka nafasi yake aliyokuwa akiishika ndani ya chama hicho na CCM wameridhia ombi hilo rasmi.

Hayo yamewekwa wazi na taarifa zilizotolewa na Katibu wa NEC-Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole leo Mei 29, 2018 na kusema kwa pamoja wamemtakia mafanikio mema katika shughuli zake.

"Napenda kumshukuru ndugu Kinana kwa utumishi wake katika Chama cha Mapinduzi (CCM) na CCM itaendeleaq kutumia uzoefu wake katika majukumu mbalimbali ya chama kwa kadiri itakavyohitajika", imesema taarifa hiyo.

Kwa upande mwingine, Kinana wakati anatoa neno lake la kuwaaga wajumbe wa NEC amewasisitizia wajumbe hao na wana CCM kiujumla kudumisha umoja wa wanachama na chama cha mapinduzi (CCM).


Advertisement

No comments

Powered by Blogger.