Header Ads

DEREVA BODABODA AFARIKI KWA KUGONGWA NA GARI KIJIJI CHA MFUMBI WILAYANI MAKETE


Image result for RENATHA MZINGA
   Kamanda Renatha Mzinga
Mtu mmoja aliyetambulika kwa majina ya Faustin Joseph (50) Mkazi wa Chimala Mkoani Mbeya amefariki Dunia kwa ajali ya kugongwa na gari akiwa anaendesha Pikipiki(Bodaboda) Kijiji cha Mfumbi kata ya Mfumbi Wilayani Makete Mkoani Njombe

Ajali hiyo imetokea tarehe 20 May 2018 katika kijiji cha Mfumbi Wilayani Makete wakati Dereva Erasto Yona(34) mkazi wa Kimara Dar es salaam akiendesha Gari lenye namba T342 DLV aina ya Toyota ikiwa imetokea Kyela kuelekea Dar es salaam aligonga pikipiki namba T825 CAY aina ya Skaymark iliyokuwa ikiendeshwa na Dereva  Faustin Joseph na kusababisha kifo chake papo hapo na kujeruhi abiria wawili ambao ni Neema Bonifasi na Given Faustin Melele

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Renatha Mzinga ametoa taarifa hiyo na kuthibitisha kifo cha Dereva bodaboda huyo

Kamanda Mzinga amesema Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe uliosababishwa na Dereva bodaboda aliyekuwa akiingia Barabara kuu ya Mbeya-Dar bila kuchukua tahadhari

Kamanda Mzinga amewataka Madereva Mkoani Njombe pindi waendeshapo vyombo vya Moto barabarani kuchukua tahadhari na kuendesha vyombo hivyo kwa umakini na kuzingatia taratibu na sheria za usalama Barabarani ili kuepuka ajali na kusababisha vifo kwa watu wasio na hatia

Huku Jeshi hilo la Polisi Mkoani Njombe likiongeza kwamba litaendelea kutoa Elimu ya Usalama Barabarani kwa wananchi wote na kuwataka wananchi kuwa makini wanapokuwa wanatembea kwa miguu barabarani

No comments

Powered by Blogger.