MWENGE WA UHURU KUKIMBIZWA TAREHE 30 NA 31 MAY WILAYANI MAKETE MKOANI NJOMBE
Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kupokelewa Wilayani Makete Mkoani
Njombe Tarehe 30 May 2018 na kufanya shughuli mbalimbali za uzinduzi na kuweka
mawe ya Msingi katika Miradi ya Maendeleo
Taarifa iliyotolewa na Mratibu wa Mbio za Mwenge Kiwilaya
ambaye pia ni Afisa Vijana Wilaya Ndg.Bruno Mwangwale mbele ya Baraza la
Madiwani Wilaya ya Makete hii leo amesema mwenge wa Uhuru utakuwa Makete
kwa siku mbili kuanzia tarehe 30 na 31 May 2018
Mratibu wa Mbio za Mwenge Kiwilaya Ndg.Bruno Mwangwale
amesema Mwenge huo utapokelewa Kijiji cha Mfumbi Kata ya Mfumbi siku yaTarehe
30 mwezi wa Tano na mwenge huo utakesha Kijiji na Kata ya Tandala na tarehe 31
kukabidhiwa Wilaya ya Njombe
Mwenge wa Uhuru ukiwa Wilayani Makete utakimbizwa kutoka kata ya Mfumbi kuelekea kata za Matamba,Mlondwe,Kitulo,Isapulano,Iwawa,Lupalilo na Mwisho Mwenge huo utakesha Kijiji na Kata ya Tandala
No comments