HALMASHAURI YA WILAYA YA MAKETE YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Makete Ndg.Francis Namaumbo
Halmashauri ya Wilaya ya Makete Mkoani Njombe
imepongezwa kwa kupata hati safi kwa mwaka wa Fedha 2016/17 kufuatia ukaguzi wa
Mkaguzi na mdhibiti wa Hesabu za Serikali
Pongezi hizo zimetolewa hapo jana na Madiwani wa
Halmashauri ya Wilaya ya Makete kwa Mkurugenzi Mtendaji na watendaji wake wote
kwa kuongeza ufanisi katika uwajibikaji na kuipa Halmashauri sifa nzuri
ya kutokuwa na hati ya Mashaka au hati chafu
Akitoa Taarifa ya Mkaguzi na mdhibiti wa
Hesabu za Serikali Mweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Makete Edward
Mdagachule kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Makete Francis Namaumbo
mbele ya Waheshimiwa Madiwani katika kikao cha Barala la Madiwani hapo jana kilichofanyika ukumbi wa Halmashauri amesema Wilaya ya Makete kwa mwaka wa
fedha 2016/17 imefanikiwa kupata hati safi
Waheshimiwa Madiwani wametumia nafasi hiyo
kuipongeza Ofisi y Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Makete kwa utendaji kazi mzuri
pamoja na watumishi wengine walioshiriki katika kuifanya Halmashauri ya Wilaya
ya Makete kupata hati safi
Makamu Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya ya Makete Mh.Jison Mbalizi ametoa rai kwa Waheshimiwa Madiwani,Watendaji na ofisi nzima ya Mkurugenzi kuendelea kushirikiana katika mambo mbalimbali ya utendaji katika kuhakikisha hati hii inakuwa na Mwendelezo na siyo kuachiana majukumu au kuhujumiana kwenye kazi mbalimbali
No comments