Header Ads

TAKUKURU MAKETE WAAGIZWA KUCHUNGUZA MIRADI HII SHULE YA SEKONDARI MATAMBA NA SHULE YA MSINGI MANGA


Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Charles kabeho amegoma kuzindua mradi wa Vyoo vya kisasa Shule ya Sekondari Matamba kata ya Matamba Wilayani Makete

Mradi huo umegharimu Milioni 58 ukiwa umejenga vyoo 23 ambavyo Kiongozi wa Mwenge amesema ameridhika na ubora wake lakini gharama zilizotumika amezikataa kuwa hana uhakika kwa kuwa gharama ni kubwa kuliko Matundu ya vyoo ambayo ni machache


Kiongozi huo amesema vyoo hivyo vingejengwa angalau kwa Milioni moja kila tundu angeridhia lakini siyo gharama hizo zilizotumika ambazo ni zaidi ya Milioni 2.5 kwa kila tundu

Mradi huo umefadhiliwa na shirika la SAWA na ameagiza TAKUKURU Wilaya ya Makete kufuatilia uhalali wa manunuzi ya vifaa vilivyotumika na uhalisia wa fedha

Mchana huu amegoma kuzindua mradi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya Walimu Shule ya Msingi Manga ujuni kwa Madai ya mradi kuwa chini ya kiwango

Image may contain: sky, house, cloud and outdoor

No comments

Powered by Blogger.