MWANAFUNZI ASHIKILIWA NA POLISI MAKETE KWA KUTUHUMIWA KUCHOMA BWENI LA WAVULANA MANG'OTO SEKONDARI
Mwonekano wa Bweni hilo baada ya kuungua
Wananchi waliofika kushuhudia Ajali hiyo ya moto
Baadhi ya vitu vilivyookolewa
Haya ndiyo Magodoro yaliyookolewa ambayo ni manne tu
Wanafunzi shule ya Sekondari Mang'oto wakimsikiliza Afisa Elimu Sekondari Mwl.Jacob Meena aliyefika shuleni hapo na kuzungumza na Wanafunzi hao
Wananchi waliofika kushuhudia Ajali hiyo ya moto
Baadhi ya vitu vilivyookolewa
Haya ndiyo Magodoro yaliyookolewa ambayo ni manne tu
Wanafunzi shule ya Sekondari Mang'oto wakimsikiliza Afisa Elimu Sekondari Mwl.Jacob Meena aliyefika shuleni hapo na kuzungumza na Wanafunzi hao
Mwanafunzi wa kidato cha pili Mvulana (15) jina linahifadhiwa amekiri kuchoma Bweni la Wavulana shule ya Sekondari Mang'oto kwa madai kuwa amechukizwa na adhabu aliyopewa na Wanafunzi wenzake ya kupigwa baada ya kubomoa kibanda cha Mwalimu na kuiba pipi,Biskuti na karanga hapo Juzi Jumapili
Baada ya kupewa adhabu hiyo mwanafunzi huyo amesema aliamua kurudi kijijini kwao Makangalawe na jana aliporudi shule alirudi akiwa na Mpango wa kuchoma Bweni akiwa na kiberiti
Mwanafunzi huyo amesema amechoma bweni hilo mnamo saa moja jioni wakati wanafunzi wenzake wakiwa Darasani vipindi vya usiku
Wanafunzi wakiwa Darasani wakaona kama Bwenini kuna moto ndipo walipogundua tukio hilo na kupiga yowe kuomba msaada
Mwanafunzi wa kwanza kujua tukio hilo na aliyemkata Mwanafunzi huyo ameelezea alichokishuhudia na kuongeza kuwa wakati huo ndani ya Bweni kulikuwa na wanafunzi kadhaa walikuwa wamejipumzisha ambao ni wagonjwa lakini walikuwa hawajui kama nje Bweni linaungua
Afisa Elimu Sekondari Mwl.Jackob Meena amewaomba wanafunzi kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu kwao wakati utaratibu ukiendelea kufanyika ili kuwasaidia wanafunzi waliounguliwa na vifaa vyao
Wananchi waliofika kushuhudia Ajali hiyo wamesema Ajali hiyo imewasikitisha lakini wanashukuru kwamba wanafunzi wote wako salama
Diwani wa Kata ya Mang’oto Mh.Osmund Idawa ametoa pole kwa wanafunzi hao na wazazi kufuatia kutokea kwa ajali hiyo na kuongeza kuwa baada ya tathmini kufanyika yupo tayari kushirikiana na wazazi kurudisha miundombinu ya Bweni hilo
Bweni hilo linabeba wanafunzi zaidi ya 140 na ni magodoro manne tu yaliyookolewa huku vitu vingine vikiwa vimeteketea kabisa
No comments