Header Ads

WALIMU WAKUU SHULE 10 ZA MWISHO KUACHIA NGAZI LUDEWA-NJOMBE


Image may contain: 2 peopleNa Maiko Luoga

Mkuu Wa Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe Mh, Andrea Tsere Amewataka Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari Ambao Shule zao Zimeshika Nafasi za Mikia zilizopo Katika Makundi ya Shule Kumi Duni Kwa matokeo ya Darasa la Saba na kidato cha Nne mwaka 2017 Wajiuzuru Nafasi zao za Ukuu wa Shule kwa kuwa Wameshindwa Kutekeleza Majukumu yao.

Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Ametoa Maagizo hayo February 20/2018 Kwenye Mkutano wa Wadau wa Maendeleo Wilaya ya Ludewa Mkutano Uliofanyika Katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Ukiwa na Lengo Kubwa la Kujadili Kiwango cha Elimu Katika Wilaya ya Ludewa ambapo Shule za Msingi na Sekondari za Wilaya ya Ludewa kwa miaka Mitano iliyopita Zimekuwa zikifanya Vibaya Katika Matokeo yake na Kushika Nafasi za Mwisho Kimkoa.

No comments

Powered by Blogger.